Aliyekuwa waziri mkuu wa zamani na mjumbe wa kamati kuu ya Chadema, Edward Lowasa amepokelewa rasmi kurudi katika chama cha mapinduzi (CCM) na katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole
Akizungumza mara baada ya kukaribishwa rasmi, Lowassa amewashukuru Watanzania milioni 6 waliompigia kura mwaka 2015 na kuwaomba kura hizo wampe rais Magufuli
Amesema kuwa ameamua kurudi CCM kwa kuvutiwa na kazi anazozifanya rais Dkt. Magufuli hivyo amewasihi wananchi wa Monduli kumuunga mkono kwa kazi anazozifanya kwa maendeleo ya Taifa la Tanzania
”Nimerudi nyumbani, sina maneno mengi ila nasema nimerudi nyumbani, Chadema nawashukuru sana neno langu kuu nasema nawashukuru, msinilishe maneno mdomoni,”amesema Lowassa


No comments:
Post a Comment