Takukuru Manyara yawapandisha wanne kizimbani kwa kukwepa kodi - TASMARA1

TAWI LA SIMBA SPORTS CLUB MKOANI MARA

TASMARA - TASMARA - TASMARA

AHSANTE SANA NA KARIBU TASMARA

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Takukuru Manyara yawapandisha wanne kizimbani kwa kukwepa kodi

Share This

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Manyara ,imewapandisha kizimbani watu wanne kwa kosa  la kukwepa kodi.

Naibu mkuu wa Takukuru mkoa wa Manyara Isdory Kyando amesema kesi hiyo namba CC.3/2019 ilifunguliwa  Februari 22 mwaka huu katika mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Manyara.

Naibu mkuu huyo amewataja  washtakiwa,kuwa ni Nashon Odhiambo Macokecha ambaye alikuwa Afisa Wanyama Pori Halmashauri ya wilaya ya  Babati, Erasto Belela Kou Mwenyekiti wa Kijiji Vilima Vitatu, Francis Mwaso Mbele,aliyekuwa Kaimu Katibu wa Jumuhiya ya Hifadhi ya Wanyama Pori Burunge na Samson Sylvester Rumende ambaye ni Wakili wa kujitegemea.

Amesema Washtakiwa wote hao wanashtakiwa kwa kosa la kukwepa kodi K/F cha 15(b) cha Sheria ya Magari (Ushuru wa Usajili namba 124/2006).

Aidha amesema  mshtakiwa wa nne Samson Sylvester Rumende  Wakili wa kujitegemea anashitakiwa kwa kosa la Kughushi K/F 333, 335(d)(i) na 337 vyote vya Kanuni ya Adhabu.

Washtakiwa walikana makosa yote.

Mshtakiwa wa pili na wanne walidhaminiwa, Mshtakiwa wa kwanza na watatu hawakuweza kufika mahakamani hivyo Mahakama imetoa hati za wito wahudhurie April 4 mwaka huu ambapo shauri limepangwa kwa ajili ya kutajwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here