Ligi ya mabingwa ulaya: Ajax imeichapa Real Madrid nyumbani - TASMARA1

TAWI LA SIMBA SPORTS CLUB MKOANI MARA

TASMARA - TASMARA - TASMARA

AHSANTE SANA NA KARIBU TASMARA

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Ligi ya mabingwa ulaya: Ajax imeichapa Real Madrid nyumbani

Share This

Dusan TadicHaki miliki ya picha

Ajax ikicheza soka la kiwango cha hali ya juu, imefanikiwa kuiondosha mabingwa wa ulaya mara 13, Real Madrid katika uwanja wake wa nyumbani Bernabeu na kufuzu kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 22.
Ikilala 2-1 katika mchezo wa kwanza, kikosi cha Erick ten Hag kilipata magoli ya mapema ndani ya dakika 18 kupitia kwa mshambuliaji wake Hakim Ziyech na David Neres.
Kiungo wa timu hiyo Dusan Tadic, alitengeneza mabao mawili , na kufunga goli la tatu kwa timu yake ya Ajax.
Real Madrid iliyokuwa inasaka taji la nne mfululizo la michuano hiyo, ilizinduka kwa goli la Marco Asensio katika dakika 20 za mwisho.
Lakini kiungo wa Ajax Lasse Schone kupitia mpira wa adhabu dakika mbili baadae , aliwanyamazisha vijana wa Santiago Solari ambao walihitaji kufunga magoli matatu zaidi ili kusonga mbele.
Gareth Bale ambaye alizomewa na mashabiki katika mchezo wa jumamosi dhidi ya Barcelona, aliingia dakika ya 29 kuchukua nafasi ya Lucas Vazquez aliyeumia .
Mkosi uliendelea kuwakumba Real Madrid ambapo nyota wake Nacho alipewa kadi nyekundi katika dakika za lala salama.
Kwa ushindi huo Ajax inakuwa timu ya kwanza kufungwa nyumbani katika mchezo wa kwanza na kufanikiwa kupindua matokeo kwenye michuano ya ulaya.
Mchezaji bora wa mechi- Dusan Tadic (Ajax)

Dusan TadicHaki miliki ya picha
Image captionMshambuliaji wa Ajax Dusan Tadic alikuwa nyota wa mchezo akiongoza mashambulizi ya Ajax dhidi ya Madrid.Akitengeneza magoli mawili na kufunga moja na kupiga pasi tano za uhakika.

  • Real Madrid inakuwa bingwa mtetezi wa kwanza kushindwa kufuzu hatua ya robo fainali ya klabu bingwa ya ulaya tangu Chelsea ifanye hivyo msimu wa 2012-13.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here